We have reached more than 10000+ Youth, it is a time for uniting and come together to overcome several challenges including Unemployment, If you interested ?

Kongamano La Vijana na Mwl. Nyerere

Moja ya picha ya pamoja ya Sisi Tanzania pamoja na Jatu plc,  waandaaji wa Kongamano la Vijana na Mwalimu Nyerere lililofanyika Jana Tarehe 14/10/2021 Ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete conventional center katika kuadhimisha miaka 22 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, ambapo mgeni rasmi alikuwa  Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mhe. Joseph Butiku, ambaye pia alikuwa Katibu wa Mwl.Nyerere enzi za uhai wake.
Huku akiambatana na Mbunge Kijana wa Dodoma Mjini Mhe. Anthony Mavunde akiambatana na  wabunge wengine wakiwemo Mh. Festo Sanga, Mhe. Nusrat Hanje, Mhe. Neema Lugangira, Mhe. Judith Kapinga, Mhe. Humphrey Polepole kuwataja wachache.
Taasisi na mashirika mbalimbali yalihudhuria mkutano huu, wanafunzi wa vyuo, wahadhiri, wanafunzi wa sekondari,  wajasiriamali na wananchi  wengine.

Oct 16, 2021